Wiki kadhaa baada ya shirikisho la soka duniani kutuma ujumbe wake kuja kufuatilia suala la uchaguzi mkuu wa TFF uliogubikwa na matukio kadhaa ya utata, leo hii shirikisho hilo la soka duniani limetoa maamuzi ya mchakato wote wa uchaguzi mkuu wa TFF kuanza upya, kwa maana wale wagombea wote waliokatwa wanaweza kurudi kwenye mchakato wa uchaguzi.
Taarifa nilizonazo FIFA imeshatuma barua ya kuelezea uamuzi kwa TFF na muda mchache ujao TFF inatarajiwa kutoa taarifa rasmi kuhusu uamuzi huo wa FIFA.
Endelea kuwa nasi kwa taarifa kamili
0 comments:
Post a Comment